Apr 23, 2014

Viwiliwili vya mauaji ya umati vyapatikana S/ Kusini

Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa malundo kwa malundo ya viwiliwili vimetelekezwa baada ya kujiri mauaji ya umati huko Sudan Kusini wiki iliyopita. 

Toby Lanzer Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na misaada ya kibinadamu amesema kuwa viwiliwili vingi vya wahanga wa mauaji hayo viko misikitini na hospitalini na kutelekezwa huko katika mji wa Bentiu, makao makuu ya mkoa wa Unity unaozalisha mafuta nchini Sudan Kusini, baada ya kabila la Nuers kufanya mauaji ya umati tarehe 15 na 16 mwezi huu.
 
Lanzer amesema hii ni mara ya kwanza kuwa na taarifa kwamba, kituo cha redio cha kieneo kilikuwa kikitangaza ujumbe wa chuki unaowahimiza watu kushiriki katika uovu huo. 

Ameongeza kuwa maelfu ya wakimbizi kutoka makundi tafauti ya kikabila wanakimbilia kwenye makao makuu ya kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa huko Bentiu kwa ajili ya hifadhi, huku wengine wengi wakiamini kuwa machafuko zaidi yanakuja. 

Kituo hicho cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kinawahifadhi watu 22, 000. 

0 comments:

Post a Comment