Sep 27, 2013

Dunia Imebadilika- Sheikh Omar

SHEIKH OMAR AL HAD OMAR WAKATI AKIZUNGUMZA LEO HII MARA BAADA YA SWALA YA IJUMAA.

Imeelezwa kwamba Dunia imebadilika na wakati tuliopo sasa si ule wakati uliopita.

Hayo yamesemwa na Imamu wa Msikiti wa Kichangani Sheikh Omar Alhad Omar.

Ameyasema hayo leo hii alipokuwa anazungumza na Waumini wa msikiti huo muda mfupi baada ya Swala ya Ijumaa.

Amesema "Kila nyanja imebadilika si ile ya zamani,ukiangalia mfumo wa Biashara,au mfumo wa Elimu na kadhalika umebadilika kwa kiasi kikubwa,kwa bahati mbaya sana sisi Watanzania ndiyo tumekuwa wa mwisho kugundua na kufuata mabadiliko katika kila sekta"

Aliendelea kwa kusema "hata viongozi wanapaswa walijuwe hili,kwamba wanawajibika kuongoza kwa mujibu wa zama tuliyo nayo lakini pia kwa mujibu wa uadilifu,tukio lililotokea kenya wiki iliyopita ni tukio la kujifunza mengi lakini mafunzo moja wapo ni kwamba dunia imebadilika".mwisho wa kumnukuu

Aidha alionyesha masikitiko yake kwa Waislamu wa Tanzania kutokujuwa nafasi yao.

Wakati huo huo michango inayoendelea kuchangwa katika msikiti wa Kichangani imefikia shilingi milioni tano.

Ifuatayo ni Takwimu ya mapato (Tunayo nakala ya mchanganuo huo) tuliyoipata mara baada ya Swala ya Ijumaa leo hii.

Tarehe 13/9/13      420,800/-
Tarehe  14/9/13       63,750 (mchango wa umeme),
Tarehe  15/9/13     115,200/-
Tarehe  16/9/13     141,200/ kuwachangia watoto wanne,
Tarehe  17/9/13      230,000/-
Tarehe  18/9/13      132,000/-  (mchango wa umeme),
Tarehe  19/9/13      209,500/-
Tarehe   20/9/13     453,000/-
Tarehe   21/9/13       81,000/-
Tarehe   22/9/13     131,500/-
Tarehe   23/9/13     173,900/-
Tarehe  24/9/13      172,100/-
Tarehe  25/9/13        57,400/-
Tarehe  26/9/13        55,800/-  
Jumla ya Pesa yote tangu kuanza kwa michango hiyo September 2 hadi kufika jana tarehe 26/9/13 ni Shilingi 5,422,200


0 comments:

Post a Comment