WAKILI wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold
Sungusia amesema baadhi ya watu wamekuwa na tabia ya kuwateka watoto
kwa lengo la kutaka wazazi wao watoe fedha ili waweze kuwakomboa.
Sungusia alisema hayo katika maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu
Kimataifa na miaka 65 ya Tamko la Haki za Binadamu Duniani,
yaliyoadhimishwa juzi na LHRC, jijini Dar es Salaam.
Kutokana na hali hiyo, aliwatahadharisha watoto kuepuka lifti na
mazingira hatarishi ambayo yanaweza kuwaweka katika mazingira ya
kutekwa.
Akizungumzia haki za watoto, alisema watoto 127 kati ya Januari hadi
Juni mwaka huu walizaliwa, wakatupwa au kutelekezwa, hali inayoonyesha
kila siku kuna mtoto anatupwa.
Pia alisema katika kipindi cha miezi sita watoto 394 walilawitiwa.
Awali Mkurugenzi wa LHRC, Helen Kijo Bisimba, alizitaka mamlaka
zinazohusika zisizime haki za watu ili nchi iendelee kuwa na amani na
utulivu.
Dec 12, 2013
WATOTO MUSIPENDE LIFTI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)





0 comments:
Post a Comment