Aug 16, 2014

Watu 34 wauawa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati

Watu 34 wanaripotiwa kuuawa katika kaskazini mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati baada ya watu waliokuwa na silaha kufanya mashambulio katika kijiji kimoja.
 Afisa mmoja wa vikosi vya kusimamia amani vya Umoja wa Afrika katika Jamhuri ya Afrika ya Kati MISCA ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kwamba, watu wengine kumi wameuawa katika shambulio hilo. 

Taarifa zaidi zinasema kuwa, shambulio hilo limetokea kilomita 400 kaskazini mwa mji mkuu Bangui. Wakati huo huo, Askofu Mkuu wa Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ametoa wito wa kuharakishwa mchakato wa kuundwa serikali mpya sambamba na kuongezwa juhudi za kuhitimisha masaibu yanayowakabili wananchi wa nchi hiyo.

Dieudonne Nzapalainga amesisitiza kwamba, kuna haja ya kuchukuliwa hatua za haraka za kuhitimisha mgogoro wa nchi hiyo. 

Kushtadi mapigano ya kikabila baina ya makundi ya wanamgambo tangu mwezi Disemba mwaka jana kumeifanya Jamhuri ya Afrika ya Kati kuwa nchi ya machafuko na isiyo na amani huku Waislamu wakiwa waathirika wakubwa zaidi wa machafuko hayo.

0 comments:

Post a Comment