Feb 21, 2015

Gazeti la Kizayuni lamvunjia heshima Mtume SAW

Wananchi wa Palestina wa ardhi zilizoanza kukaliwa kwa mabavu mwaka 1948 na kupewa jina la Israel wamelaani kitendo cha gazeti la Kizayuni la Yediot Ahronot cha kuchapisha katuni zinazoitusi na kuivunjia heshima shakhsia tukufu ya Bwana Mtume Muhammad SAW.
Vyama vya Waarabu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni tangu mwaka 1948 leo vimetoa taarifa ya pamoja, ambapo mbali na kulaani kitendo cha gazeti la Kizayuni la Yediot Ahronot cha kuchapisha vikatuni vya kumkejeli na kumvunjia heshima Bwana Mtume SAW vimeeleza kuwa lengo la hatua hiyo, bila ya shaka yoyote ni kuchochea hisia za Waislamu. 

Hapo kabla pia magazeti ya utawala wa Kizayuni wa Israel yaliwahi kuchukua hatua za kumvunjia heshima Bwana Mtume Muhammad SAW…/

0 comments:

Post a Comment